Rais wa Ujerumani awahakikishia wananchi kuhusu COVID-19

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Rais wa Ujerumani, Frank-Walter Steinmeier amewahakikishia wananchi wa Ujerumani kwamba janga la virusi vya corona haliwezi kuuondoa mustakabali wao. 
Katika barua yake iliyochapishwa kwenye gazeti la Bild am Sonntag, Steinmeier amesema maendeleo kuhusu utafiti yanatoa matumaini kwamba janga la COVID-19 halitoyatawala maisha yao milele. 

Taasisi ya kudhibiti magonjwa ya kuambukiza ya Ujerumani, Robert Koch imethibitisha maambukizi nchini humo yameongezeka hadi watu 14,611 jana Jumapili. Wizara ya afya ya Ujerumani imesema chanjo ya virusi vya corona inaweza kuidhinishwa katikati ya mwezi Desemba. 

Nchini Marekani, mkuu wa kitengo cha magonjwa yanayoambukiza Dokta Anthony Fauci, amesema maambukizi yanaweza kuongezeka wiki zijazo kutokana na sherehe za kutoa shukrani, Thanks Giving. 

Aidha, Korea Kaskazini inajenga ukuta karibu na mpaka wa Korea Kusini na inaimarisha ulinzi kwenye maeneo ya pwani ili kuzuia virusi vya corona kuingia nchini humo.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad