AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv
MSHAMBULIAJI wa Timu ya Taifa ya Tanzania na Fenerbache, Nahodha Mbwana Ally Samatta atakuwa nje ya dimba kwa muda wa siku 10 baada ya kuumia.
Samatta amepata maumivu ya misuli katika mchezo wake wa mwisho wa Ligi ya Uturuki dhidi ya Konyaspor wakipoteza kwa goli 2-0.
Baada ya maumivu hayo, Samatta ataukosa mchezo wa kufuzu AFCON kati ya timu yake ya Taifa Tanzania dhidi ya Tunisia utakaochezwa Novemba 13 na Novemba 17 mwaka huu.
Kwa upande wake Samatta amesema, aliumia katika mechi ya mwisho ya Ligi na alipata maumivu ya misuli na nilifanyiwa vipimo na majibu yametoka mabaya kwahiyo atakuwa nje kwa siku zaidi ya 10.
Amesema, ripoti ya daktari inaelezea kuwa anatakiwa apumzike ili misuli irejee katika hali ya kawaida.
Samatta ametoa ya moyoni na kusema, ameumizwa sana kuukosa mchezo huo muhimu kwani alitamani awepo uwanjani kama kiongozi wa timu ila haina jinsi na ameenda kuongea na vijana wa timu pamoja na viongozi ili kuwapa morali ya ushindi.
Kwa sasa timu ipo nchini Uturuki ikijindaa na mchezo wao wa kufuzu AFCON dhidi ya Tunisia.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK