Viongozi wa Al- Shabaab wapigwa marufuku kuingia Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Marekani imewawekea vikwazo viongozi wawili waandamizi wa kundi la kigaidi la Al-Shabab waliohusika na utekelezaji wa shambulio la kigaidi katika kambi ya jeshi nchini Kenya.

Afisa mmoja wa jeshi la Marekani na wanakandarasi wawili waliuawa mnamo mwezi Januari katika shambulio lililtokea kambi ya Simba kisiwa cha Manda.


Hilo lilikuwa shambulio la kwanza kutekelezwa na kundi la Al-Shabab dhidi ya jeshi la Marekani nchini Kenya.


Wizara wa Mambo ya Nje Marekani imesema kuwa imewatambua Abdullahi Osman Mohamed na Maalim Ayman katika orodha ya magaidi wa kimataifa.


Taarifa kutoka wizara hiyo imesema Bwana Mohamed ni mtaalamu mwandamizi wa vilipuzi wa kundi la Al-Shabab na kiongozi wa mausala yao ya mawasiliano huku Bwana Ayman akihusishwa na kupanga shambulizi lililotokea katika kambi ya Simba.


"Raia wa Marekani wamepigwa marufuku kujihusisha na shughuli za muamala za aina yoyote na Mohamed and Ayman. Mali zao nchini Marekani zimezuiwa," Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad