Yanga Yaridhishwa na Kiwango Cha Mukoko, kumuongezea mkataba Kabla Nyakunyaku Ajamnasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


 MABOSI wa Yanga wameweka wazi kuwa watamuongezea mkataba kiungo bora ndani ya Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020/21 kwa mwezi Oktoba, Tonombe Mukoko anayetajwa kuingia anga za Simba.

Ikiwa watamuongeza mkataba nyota huyo watazima ndoto za watani zao wa jadi kuipata saini ya kiungo huyo ambaye ni miongoni mwa wanaofanya vizuri kwa msimu wa 2020/21 na kuingilia kati dili hilo kibabe.


Mukoko aliibuka ndani ya Yanga kwenye dirisha kubwa akitokea Klabu ya AS Vita ya Congo pamoja na mwenzake Tuisila Kisinda ambao kwa pamoja wamekuwa na pacha matata ndani ya uwanja.


Kwa msimu huu pacha yao imekuwa na moto ambapo kwenye Dar Dabi, Kisinda alisababisha penalti iliyofungwa na Michael Sarpong huku Mukoko akisepa na tuzo ya mchezaji bora wa mchezo huo ikiwa ni dabi yao ya kwanza.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad