Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbasi amezungumza kuhusu Kifo cha Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mungereza, Kupitia ukurasa maalum (@msemajimkuuwaserikali) ameandika ujumbe wa mwisho kutumiwa na marehemu kabla ya kufariki Jana Alhamis
That Gal ya Rosa Ree Yawa Gumzo Itazame Hapa chini:"Nimelazwa General hapa Dom kila kitu kitaenda sawa kuhusu tamasha. Napambana." Dr. Hassan Abbasi alinukuu ujumbe huo na kusema, Ni meseji ya mwisho niliyoipokea juzi Jumanne saa tano na dakika 2 usiku kutoka kwa Kaka yangu Godfrey Mungereza, Katibu Mtendaji wa BASATA, leo hatunaye tena katika hii dunia. Ametutoka tumwombee sana, Mola ampe pumziko la amani la milele.
HABARI HIZI ZINAPATIKANA KWENYE APP YA UDAKU SPECIAL, BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD KWENYE SIMU YAKO
0 Comments