Biden Kusaini Maagizo 12 ya Rais, Kuanza na Mizozo Hii Mikubwa Minne

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Rais mteule wa Marekani Joe Biden atatia saini maagizo ya rais siku ya kuapishwa kwake kuwa rais wiki ijayo ili kushughulikia janga la virusi vya Corona, Uchumi wa nchi hiyo unaodorora, Mabadiliko ya hali ya hewa na Ubaguzi wa rangi.

Haya ni kwa mujibu wa mkuu wa utumishi anayetarajiwa Ron Klain. Katika taarifa aliyoitoa jana Jumamosi, Klain amesema kuwa mizozo yote hii inahitaji kushughulikiwa kwa haraka na kuongeza kuwa Biden atatia saini takriban maagizo 12 ya rais baada ya kuapishwa siku ya Jumatano.


Klain aliongeza kuwa katika siku zake 10 za kwanza ofisini, Biden atachukua hatua madhubuti kushughulikia mizozo hiyo minne, kuzuia madhara mengine ya haraka na yasiyoweza kurekebishwa, na kurudisha nafasi ya Marekani ulimwenguni.


Joe Biden anatarajiwa kuapishwa Januari 20, 2021 kuwa Rais wa 46 wa taifa la Marekani.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad