Mkuu wa jeshi la UPDF awaomba radhi waandishi Uganda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mkuu wa jeshi la UPDF Jenerali David Muhoozi ameomba msamaha kwa wandishi wa habari kufatia tukio la jana wakati poilisi wa jeshi la UPDF waliwatandika wandishi habari waliokuwa wakimsubiri kiongozi wa chama cha NUP Robert Kyagulanyi, aliyepeleka malalamiko yake kwenye Kemisheni ya haki za binadamu ya Umoja wa mataifa Kololo.
Jenerali David Muhoozi amesema uchunguzi umeanza kwa waliofanya kitendo hicho na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Jeshi litalipa gharama za matibabu ya wandishi habari hao.Wandishi waliojeruhiwa ni Cliff Wamala wa NTV, Josephy Dhabiti NBC,Rashid Nakayi GalaxyFm, Timoth Murungi New Vision, Irene Abaro Monitor, Josephine Namakumbi NBS na Jeff Twesigye NTV.

Jenerali Muhoozi amesema jeshi la UPDF halikuwatuma wanajeshi hao kuwapiga waandishi wa habari.

Ametoa wito kwa waandishi habari kuwa na vitambulisho vinavyoonesha wakiwa kazini kusaidia kuwatambua na mwisho amesema watafanya mpango kuzungumuza na waandishi wa habari ili kuboresha mahusiano kati ya pande hizo mbili.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad