Laana ya Fahyma kwa Rayvanny

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




BABY mama wa mkali wa Bongo Fleva kutoka Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB), Raymond Mwakyusa ‘Rayvanny’, Fahyma ‘Mama Jayden’ ameweka wazi kuwa yeye na mzazi mwenzake huyo, hali si shwari.

 

Hii ni baada ya kuwepo kwa madai kuwa ndoa ya wawili hao ilishavunjika na ndoa maana jamaa huyo akatua kwa mtoto wa mwigizaji Kajala Masanja, Paula Paul.

 

Kwa wiki kadhaa sasa, Fahyma amekuwa akitoa malalamiko yake dhidi ya Rayvanny, jambo ambalo linatafsiriwa kuwa inaweza kuwa laana kwa jamaa huyo.

 

Fahyma anasema kwamba, ni kweli kwamba yeye na Rayvanny wameachana huku akidai kwamba msanii huyo amekuwa muongo.

 

Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram, Fahyma anasema kwamba, amesalia tu na mwanawe, Jayden, licha ya kwamba msanii huyo ni tajiri.

 

Kupitia kwa jumbe zake, Fahyma anasema kwamba Rayvanny alikuwa amesahau familia yake na kuwa njia ya muongo ni fupi.

 

“Tajiri na mali yake, maskini na mwanawe malipo ni hapa duniani.”

Katika ujumbe mwingine, Fahyma anasema kuwa, Rayvanny ameharibu familia yake kwa mikono yake mwenyewe na ipo siku Mungu atamkumbusha.

 

Ujumbe wake mwingine ulisoma;

“Nimekubali kutukanwa, kubeba maumivu yote nikijua navumilia kwa mtu ambaye najua ni wa muhimu kwangu, kumbe najidanganya mwenyewe.

 

Imetosha, sasa siwezi tena, endelea na huo mchezo ambao hauna mwisho na sitaki.”

Mama huyo aliweka wazi kwamba ametosheka kudanganywa na kwamba njia ya muongo ni fupi.

Kwa upande wake, Rayvanny anakiri kutengana na Fahyma na sasa anajivinjari na Paula.

 

Stori: MEMORISE RICHARD, DAR

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad