Ajipiga risasi baada ya kuwauwa sita katika sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mwanaume mmoja mwenye silaha ajiuwa kwa risasi baada ya kuwapiga risasi na kuwaua watu sita katika sherehe za kumbukumbu ya kuzaliwa huko Colorado Springs siku ya Jumapili, polisi wameeleza.

Milio ya risasi ilisikika katika bustani ya nyumbani ambayo inahamishika ambapo familia ilikutana kusheherekea.

"Mshukiwa ambaye ni mpenzi wa msichana aliyekuwa anasheherekea siku yake ya kuzaliwa , alifika nyumbani hapo na kuanza kupiga risasi watu waliokuwa katika sherehe hiyo kabla ya kujiua yeye mwenyewe," idara ya polisi ya Colorado Springs imesema.

Sababu ya shambulio hilo halijafahamika mpaka sasa.

Watu wote waliopigwa risasi walikuwa watu wazima ingawa kulikuwa na watoto katika sherehe hiyo katika wakati huo.

Hawajatajwa majina watu waliopigwa risasi na hata mshambuliaji hajatajwa bado.

"Tukio la kikatili limepelekea watu sita kufariki na wengine kujeruhiwa.Watoto hawakujeruhiwa na mshukiwa huyo na wapo na ndugu zao sasa,"polisi wameeleza.

Meya wa Colorado Springs Mayor John Suthers ametaja kuwa uhalifu huo ambao hauna maana; Leo tumejikuta tunaomboleza kupoteza kwa wapendwa wetu na kuwaombea wale waliojeruhiwa kupona haraka na familia zilizopoteza wapendwa wao."

Mwezi Machi, watu 10 waliuawa katika shambulio la risasi ndani ya duka katika mji ulio mpakani mwa Colorado. Mshukiwa alikamatwa baadae na kukabiliana na mashtaka 10 ya mauaji.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad