Nigeria yafungia Mtandao wa Twitter Kisa Tweet ya Rais Kufutwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Serikali ya Nigeria imetangaza kuufungia mtandao wa Twitter nchini humo. Waziri wa Mawasiliano na Utamaduni, Lai Mohammed amesema uamuzi huo umetokana na kuwepo na kujirudia kwa matumizi ya mtandao huo katika kushusha hadhi ya nchi hiyo.


Uamuzi huu unakuja ikiwa ni siku moja baada ya Twitter kufuta tweets na video za Rais wa nchi hiyo Muhammadu Buhari akitoa onyo la adhabu kwa kikundi cha IPOB akikishutumu kwa mashambulizi katika majengo ya Serikali. Twitter ilisema imefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa tweet hizo zilikiuka kanuni za matumizi ya mtandao.


Sambamba na uamuzi huo, Serikali ya Nigeria imeiagiza Tume ya Taifa ya Utangazaji (NBC) kuanza mchakato wa kutoa leseni kwa mitandao yote ya kijamii inayotoa huduma ya kurusha video nchini humo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad