Kanye West ashirikiana na hasimu wake Jay-Z katika albamu yake mpya Donda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Kanye West amefichua kwamba Jay-Z ni miongoni mwa wasanii walioshiriki katika albamu yake mpya alioizindua.
West aliandaa sherehe ya albamu hiyo ya Donda -aliyoipatia jina la mamake ambaye ni marehemu katika uwanja uliofurika wa Mercedes Benz , mjini Atlanta katika jimbo la Georgia , mji aliozaliwa.

Akivalia jaketi la rangi nyekundu , lililofanana na suruali aliyovaa na viatu vya rangi ya machungwa zote zikiwa na nembo yake, Yeezy Mogul,44 , usoni alivalia kile kilichoonekana kuwa barakoa iliotengenezwa na mpira.

Aliingia katika ukumbi bila kusema na albamu ikaanza kuchezwa bila utangulizi rasmi kutoka kwa mtengenezaji wake.

Wimbo wa mwisho ulimshirikisha Jay-Z, rafiki yake wa siku nyingi , mpinzani na mshirika wake.

Mshororo mmoja wa Jay-Z ulishirikisha neno ‘’red cap’’ – akimaanisha kofia ya Kanye West ilioandikwa MAGA {‘Make America Great Again’}.

Young Guru, mzalishaji wa muziki na muhandisi ambaye amefanya kazi na Jay-Z , alifichua kwamba mshororo huo uliongezwa dakika za mwisho , pengine akielezea kwanini sherehe hiyo ilichelewa kwa saa mbili.

Alituma ujumbe wa twitter: ‘’HOV aliimba mshororo huo hii leo!!! Saa 10 jioni’’.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad