Mwanariadha wa Uganda afurushwa Japan

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mnyanyuaji uzani wa Uganda aliyetoweka katika kambi ya Olimpiki magharibi mwa Japan Ijumaa iliyopita amerejea nyumbani saa chache kabla ya kuanza rasmi kwa michezo ya Olimpiki.

Julius Ssekitoleko alirejeshwa nyumbani leo asubuhi na kuchukuliwa na polisi muda mfupi baada ya kutua katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Entebbe.

Mama yake mzazi, mke wake mjamzito na maafisa wengine wa serikali waliokuwa wamesafiri kumlaki hawakufanikiwa kumuona.

Katika taarifa, Wazara ya Mambo ya Nje ilisema, "Serikali ya Uganda imejitolea kuendelea kumhudumia mwanariadha huyo ili kumsaidia atulie na kuendeleza kazi yake lakini pia kumsaidia kuelewa jinsi vitendo kama hivi vibaya havimuathiri yeye tu kama mwanariadha lakini pia wanariadha wengine katika sekta ya Michezo na taifa kwa ujumla. "

Wakati alipotoweka katika chumba chake cha hoteli huko Izumisako mjini Osaka, Julius alikuwa hajatimiza viwango vya Olimpiki vilivyowekwa kimataifa alipofika Japan.

Alitakiwa kurejea nyumbani Uganda katikati ya wiki hii.

Aliacha kijikaratasi chenye ujumbe pamoja na mizigo yake akisema anataka kubaki Japan na kufanya kazi.

Polisi wa Japan walimpata Julius katika mji wa Yokkaichi, maili 105 kutoka kambi wa wachezaji wa Olimpiki.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad