Miili ya Watumishi Watano TRA Yaagwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Vilio na majonzi vimetawala hii leo Agosti 24, 2021, katika viwanja vya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani Mbeya, wakati wa kuaga miili ya wafanyakazi watano wa TRA kikosi kazi cha fast track waliofariki dunia hapo jana kwa ajali ya gari mkoani Songwe.

Ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Hanseketwa Wilayani Mbozi Mkoani Songwe majira ya saa 11 alfajiri jana Agosti 23, 2021 baada ya gari lao aina ya Landcruiser yenye nambari za Usajili STL 8825 Mali ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambalo liligonga Lori aina ya FUSO yenye nambari za usajili T 586 ANE.

Watumishi wa TRA waliofariki ajalini ni Azari Shifonike ambaye ni dereva, Joel Mitondwa, Saidi Buddy, Fahad Hassan na Benard Mashingi. Miili yao itasafirishwa kwenda mikoa mbalimbali ambako kila mmoja ni nyumbani kwao kwa ajili ya mazishi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad