Msanii wa Bongo Fleva @officialnandy amewashtua na kuwashangaza wengi mashabiki na wanachama wa Yanga kwa kuingia Uwanja wa Mkapa kwa staili ya kipekee na kufanya ‘Show’ iliyowavutia waliyowengi. @officialnandy aliingia Uwanjani akiwa ndani ya ‘BOKSI’ huku akibebwa na mabaunsa walioshiba hasa kutokana na ukubwa wake .