Kaze "Nimekuja Kuipa Ubingwa Yanga SC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




KOCHA Msaidizi wa Yanga, Cedric Kaze, amesema ametua kikosini hapo kuipa mataji, huku akisisitiza atashirikiana kikamilifu na kocha mkuu, Nasreddine Nabi.

Kaze amewahi kuwa Kocha Mkuu wa Yanga msimu uliopita ambapo alifanikiwa kuipa Kombe la Mapinduzi kabla ya kusitishiwa mkataba wake na nafasi yake kuchukuliwa na Nabi.

Akizungumza na Spoti Xtra, Kaze alisema: “Ninafuraha kubwa kuona nimerudi ndani ya Yanga nikiwa kama kocha msaidizi, hivyo malengo ya timu ndio malengo yangu pia, nipo katika sehemu ya malengo ya timu ambayo ni kuhakikisha tunatwaa ubingwa wa ligi kuu.

“Hivyo nikishirikiana na Kocha Mkuu, Nabi naamini malengo yatafanikiwa japo hakuna safari ambayo haina mabonde na milima, tutapambana kuhakikisha changamoto zote tunazitatua ili tufanikiwe.”

Wakati Kaze akisema hivyo, Kocha wa Viungo wa Yanga, Helmi Gueldich, ametamba kuwa wana matumaini makubwa kikosi chao kitakuwa tishio zaidi msimu huu.

“Tumefanya usajili bora kwa ajili ya msimu huu, lakini pia tuna benchi bora la ufundi hasa baada ya kuwepo maboresho kwa kuongeza baadhi ya wakufunzi akiwemo Kaze na Zahera (Mwinyi), tuna matumaini ya kuwa na kikosi tishio zaidi,” alisema.

PICHA: MUSA MATEJA
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad