AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
SERIKALI imesema rada nne za kuongozea ndege zilizofungwa katika viwanja vinne vya ndege zimesaidia kuongeza idadi ya ndege zinazotua na kuruka pamoja na mapato yatokanayo na tozo za kutumia anga la Tanzania.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini hapa alipofanya ziara katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali ikiwamo kuangalia rada ya kuongoza ndege inavyofanya kazi.
Alisema serikali imewekeza fedha nyingi kununua rada hizo ambazo zimefungwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), Songwe na Mwanza na kwamba uwekezaji huo umeanza kuleta matunda.
Kadhalika alisema kwa sasa rada hizo zinasaidia kuona ndege zote zinazopita katika anga la Tanzania na zote zinalipa tozo za serikali.
Aliwapongeza vijana wa kitanzania wanaoongoza rada hizo na kwa sasa nchi inajiongoza yenyewe, badala ya kutegemea wataalamu kutoka nje ya nchi.
"Nimeenda Songwe, Dar es Salaam, Kilimanjaro na hapa Mwanza kwa kweli nimeona serikali ilivyofanya uwekezaji katika usafiri wa anga," alisema.
Waitara alisema rada hizo pia zimesaidia ulinzi wa nchi kwa kuwa zinaona kila kitu kinachokatiza katika anga la Tanzania.
Kuhusu mapato, Waitara alisema yamepanda licha ya kuwapo ugonjwa wa Covid-19 katika nchi mbalimbali duniani.
Kwa upande wake, Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza, Pascal Kalumbate, alisema sekta ya utalii kwa sasa imeimarika wanapokea ndege nyingi uwanjani hapo.
Pia kwa sasa ulinzi katika uwanja huo umeimarika kutokana na kufungwa mtambo huo unaofanyakazi saa 24 kwa siku.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK