DC Lushoto asema waliotafuna fedha Zahanati ya Mziragembei kuzitapika, Mbunge Shekilindi apigilia 'Msumari'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mkuu wa Wilaya  ya Lushoto Mkoani Tanga Kalisti Lazaro  ameahidi  kuchukua hatua kali  za kisheria  kwa  Watumishi  watakaobain goika  kushiriki  kubadili matumizi  ya fedha  za zahanati ya Mziragembei na kuzipeleka  kwenye uchaguzi  wa Serikali za mitaa uliopita.

Hayo  aliyasema  kwenye  mkutano  wa hadhara  uliofanyika  katika   Kijiji cha Kwekanga  muda  mchache  baada ya  kutembelea  zahanati  ambayo  imejengwa  miaka  17  iliyopita  lakini  haijakamilika na  wananchi  wanaendelea  kukumbana  na changamoto  ya   kutembea  umbali mrefu  kwenda  kutafuta huduma za  afya.

Mkuu wa Wilaya  huyo  alisema  fedha  zimeletwa ili  zahanati  imalizike  lakini  baadhi   ya  viongozi kwa kushirikiana  na  kamati  ya maendeleo  ya kata  wakaamua  kubadilisha  matumizi   ya fedha kwa  kuzigawa  kwa  kila  Kijiji  kwaajili ya uchaguzi  huo wa serikali  za mitaa.

“ Wale  wote  walioshiriki  kutoa  kibari  cha  kubadili matumizi  na  kuzigawa  fedha  hizo  za zahanati  watazitapika  kwani Sheria  ya fedha  inataka  fedha  inayoletwa  kwaajili  ya mradi itumike kweye  mradi  husika yaani  hata  kama amechaguliwa  atazitapika na  nitaonyesha mfano’’ Alisema Mkuu huyo  wa  Wilaya

Lazaro  alisema  kuwa  yeye kazi  iliyomleta  ni  kusimamia  miradi  ya maendeleo  hivyo  hayuko tayari  kuona fedha ya serikali  ikitafunwa  au ukibadilishwa matumizi  wakati  mradi  husika  haujaisha  nakuongeza  kuwa  hakuna  kiongozi mkuu kwenye fedha  za serikali.

Mkuu  huyo wa wilaya  alisema  mifuko  ya jimbo  kwa  wilaya  ya lushoto  haitendewi haki  inahujumiwa sababu  hata  kule  bumbuli  kuna mil tano  iliyokuwa  imepangiwa Kwenye miradi ya maendeleo kule Kijiji cha Yamba  lakini  hazikutumika  zikarudishwa  hazina  hii  inasikitisha  kwakweli

Alisema  pia  maelezo  aliyopewa  ya matumizi  ya fedha yaliotumika  kwenye  zahanati  hiyo mpaka  sasa yanakinzana  na maelezo  aliyoyatoa Mbunge wa jimbo  hilo Shabani Shekilindi  wakati akimpa taarifa  namna  serkali kuu na mfuko  wa jimbo  na fedha  binafsi  zilivyotumika.

Awali  akisoma taarifa Mtendaji  wa Kijiji hicho mbele ya Mkuu huyo  wa wilaya  na mbunge ilionesha   kuwa  mfuko  wa jimbo  umechangia  mil 1.4  nguvu  za wananchi  sh million 6  na  ofisi  ya Mkurugenzi iliwapatia mifuko 20 ya saruji .

Kwa  upande  wake  Mbunge wa jimbo hilo  Shabani  Shekilindi  maarufu  kama  Bosnia  alisema  zahanati  hiyo  ni kati  ya  zahanati  ya  kwanza  kujengwa   katika kata  hiyo lakini  imekuwa  ya mwisho  kukamilika  inasikitisha kwakweli.

Mbunge huyo  alisema  kuwa   yeye  anapigana  kuhakikisha  wananchi  wanaondokana na changamoto  mbalimbali  lakini wanatokea  wajanja  wanabadilisha  matumizi , ‘’ Mkuu wa  wilaya  sitavumilia  kuona  wananchi  wangu wananyanyasika  naomba  uchukue  hatua za  kisheria  ili wananchi  wangu  wapate  huduma ya afya kwa ukaribu.

“ Miaka  mitano  iliyopita ya ubunge  wangu  nilikuwa  naipelekea  zahanati  hii fedha  za mfuko wa jimbo  lakini  zilikuwa  zinapigwa tu  hata  vifaa nikipeleka  vinapigwa  sasa  kwa kuwa  wewe mkuu wa wilaya  ni jembe naomba  uchunguze  jambo hili na ulichukulie  hatua  kali za  kisheria  ili tukomeshe  tabia hii sababu wananchi  wanapoteza  Maisha , wanajifungulia  njiani  kwa kukosa  huduma  ya afya karibu” Alisema  Mbunge huyo .

Hata  hivyo Kaimu  Mkurugenzi  wa  Halmashauri ya Lushoto  Emanueli  vuli alisema  kuwa kwa mujibu wa sheria  Mbunge anamamlaka ya kupeleka fedha kwenye  kata  na Kamati  ya Maendeleo  ya kata  WDC pia inamamlaka  yakupanga  na wao  ndo  wanavipaumbele lakini sisi kama halmashauri  tutalifanyia kazi  hili.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad