Kiongozi wa Mapinduzi Sudan Amfuta Kazi Mwendesha Mashtaka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Kiongozi wa mapinduzi yaliyofanyika wiki iliyopita Sudan, Luteni Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, amemfuta kazi Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP), Mubarak Mahmoud kufuatia kuachiliwa huru kwa watu kadhaa wanaohusishwa na utawala wa aliyekuwa Rais wa muda mrefu Omar al-Bashir.
 

Kufukuzwa kwa Mahmoud kumekuja baada ya mamlaka ya kijeshi kuwaachilia baadhi ya washirika wa zamani wa Bashir, akiwemo Waziri wake wa Mambo ya Nje Ibrahim Ghandour.

 

Kuachiliwa kwa Ghandour na maafisa wengine wa zamani huenda kukazua tetesi za kuwa majenerali wa kijeshi bado wanaendelea kumtii Bashir aliyepinduliwa Aprili 2019 na wanaweza kuwa walihusika katika mapinduzi ya Oktoba 25.

 

Kumekuwa na mashinikizo ya kimataifa kuwashawishi viongozi wa mapinduzi kuwaachia huru wanasiasa waliokuwa kizuizini na kurejesha serikali ya kiraia.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad