Msikiti mmoja nchini Afghanistan washambuliwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Bomu limelipuka katika msikiti mmoja wakati wa sala ya Ijumaa, na kujeruhi watu 15 mashariki mwa Afghanistan, ambapo wanamgambo wa ISIS wanaendesha kampeni ya machafuko.


Qari Hanif, msemaji wa serikali ya jimbo la Nangarhar, alisema bomu hilo linaonekana kuwa liliwekwa ndani ya msikiti huo katika mji wa Traili, ulioko katika eneo la milima la Spin Ghar, nje ya mji mkuu wa jimbo hilo Jalalabad.



Tangu kuchukua madaraka nchini Afghanistan miezi mitatu iliyopita, kundi la Taliban limeendesha kampeni ya kukabiliana na waasi, wakiapa kukomesha tishio la ISIS.



Makundi yote mawili yana msimamo mkali wa dini ya Kiislamu na kwa miaka mingi yamejihusisha na baadhi ya mbinu zilezile za vurugu, kama vile mashambulizi ya kujitoa mhanga. Hata hivyo, kundi la Taliban limelenga kuchukua udhibiti wa Afghanistan, huku Dola la Kiislamu likizingatia jihad ya kimataifa.



Msemaji wa idara ya kijasusi ya Taliban aliwaambia waandishi wa habari mjini Kabul siku ya Jumatano kwamba idara hiyo limewakamata karibu wapoganaji 600 wa ISIS, wakiwemo watu muhimu na wafadhili wa kifedha. Msemaji wa idara ya ujasusi, Khalil Hamraz, alisema takriban wanaharakati 33 wa ISIS waliuawa katika mapigano na vikosi vya usalama vya Taliban.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad