Watanzania 725 Wafariki kwa Corona

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



WATANZANIA 725 wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa Uviko-19 tangu ulipoingia nchini mapema mwaka jana. Idadi hiyo ni kati ya watu 26,164 waliothibitika kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo kati ya hao 25, 330 walipona.

Takwimu hizo zimetolewa leo Jumatano Novemba 10, 2021 bungeni na Naibu Waziri wa Afya, Dk Godwin Mollel wakati anajibu swali la mbunge wa viti Maalum Halima Mdee.

Katika swali la msingi Mdee ameuliza ni Watanzania wangapi wameugua Uviko-19 tangu ulipoingia nchini na akahoji Fedha kiasi gani zimetumika.

“Sh158 bilioni zimetumika kununua vifaa mbalimbali ikiwepo mitambo 19 ya kuzalisha hewa ya oksijeni yenye uwezo wa kuzalisha mitungi 20 hadi 300 ambapo mitambo saba ishasimikwa na mitambo 12 ipo katika hatua ya usimikaji,” amesema Naibu Waziri Mollel.


 
Akizungumzia gharama za upimaji amesema kipimo kwa mtu mmoja ni dola 135 ambapo Serikali inatoza dola 50 huku ikichangia dola 85 kwa kila anayepima.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad