Taliban hawakuingia Kabul kwa nguvu, niliwaita'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Aliyekuwa rais wa Afghanistan Hamid Karzai amesema kwamba aliwataka wapiganaji wa Taliban kuingia mji mkuu wa Kabul ili kuzuia ghasia na wizi.

Viongozi wa Taliban walituhakikishia kwamba wapiganaji wake hawataingia mji mkuu wa Afghan, Hamid Karzai aliambia chombo cha Habari cha AP katika mahojiano.

'Lakini rais wa zamani wa Afghanistan Ashraf Ghani aliondoka Kabul ghafla na maafisa wake wakuu na Taliban wasingepatikana'.

Mwezi Agosti mwaka huu , baada ya kuondoka kwa vikosi vya Marekani Taliban ilichukua udhibiti wa Afghanistan na kuiondoa serikali iliokuwa madarakani.


 
Mmoja baada ya mwengine wapiganaji hao walichukua udhibiti wa maeneo yanayozunguka mji wa Kabul . Wakati huo wapiganaji wa Taliban walihofiwa kuingia mji mkuu wakati wowote.

Baadaye Ashraf Ghani ghafla aliondoka Afghanistan na wapiganaji wa Taliban wakateka mji wa Kabul tarehe 15 Agosti.

Taliban ilisema wakati huo kwamba hawakuwa na nia ya kuingia mjini Kabul, lakini waliingia kuzuia ghasia na wizi katika mji huo.


Hamid Karzai alisema , "Mfumo wa serikali na vikosi vya usalama nchini Afghanistan ulikuwa umepooza . Yeye mwenyewe aliwaomba wapiganaji wa Taliban kuingia Kabul."

Je mpango uliokuwepo ulikuwaje?

Hamid Karzai aliambia mahojiano hayo kwamba yeye na Abdullah walikuwa wakiwasiliana na viongozi wa Taliban mjini Doha na mpango ulikuwa Taliban kuingia mjini Kabul kwa misingi ya makubaliano na serikali iliokuwepo madarakani.

"Mimi na Abdullah tulikuwa na mipango ya kuzuru Doha tarehe 15 mwezi Agosti kufanya uamuzi wa mwisho wa kisiasa na wapiganaji wa Taliban, alisema.

Kulingana na Karzai ilikuwa wakati wa mchana ambapo uvumi ulienea kuhusu kuondoka kwa rais Ghani nchini humo.


 
Alipozungumza na waziri wa masuala ya ndani, ilibainika kwamba maafisa wote akiwemo afisa mkuu wa polisi mjini Kabul walikuwa wameondoka mjini humo na kwamba hakuna aliyekuwa madarakani.

Hamid Karzai anasema kwamba iwapo rais Ghani angekuwepo nchini humo kungekuwa na uwezekano wa makubaliano ya kuafikiwa na wapiganaji wa Taliban na kutengeneza mfumo fulani.

Katiba na bunge

"Afghanistan ipo chini ya udhibiti wa Taliban . jamii ya kimataifa inahitaji kufanya majadiliano na Taliban ili kuzuia hali ya kibinadamu inayoendelea kuzorota.," Karzai said.

"Mara nyengine wanachama wa kundi hilo hawaeleweki. Kwa mfano sio sawa kwamba wanawake wa Afghanistan hawafai kutoka majumbani mwao.''


Karzai alisema aliwapatia Taliban mpango wa kujiondoa katika hali waliopo sasa. Mpango huo unashirikisha kuidhinisha katiba ya aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo Mohammad Zahir Shah mbali na kupanga kamati kuu ya wabunge inayohusika kufanya maamuzi makuu serikalini.

Kamati hiyo inaweza kufanya maamuzi kuhusu serikali mpya , katiba na bendera ya kitaifa.

Hatahivyo , alisema kwamba , haki ya wanawake kufanyakazi , haki ya wasichana na wavulana kusoma na wanawake kushiriki katika kila hatua ya maisha yao ni masuala ambayo hawawezi kunyimwa na yanapaswa kulindwa.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad