No title

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



KOCHA wa Geita Gold FC, Fred Minziro ameahidi kulipa kisasi dhidi ya Yanga kwenye mchezo wao wa Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), ambao utapigwa Jumapili hii uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Akizungumza na Spotileo, Minziro amesema anajua utakuwa mchezo mgumu kutokana na ubora waliokuwa nao Yanga, lakini wamepanga kutumia udhaifu wao, ili kulipa kisasi cha kufungwa mara mbili kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.

" Ni kweli Yanga timu kubwa na kikosi chao kimeimarika sana msimu huu, lakini tumefuatilia mechi zao nyingi walizocheza hivi karibuni na kuna mapungufu tumeyaona, tumepanga kuyatumia, licha ya uzuri wao lakini wanafungika," amesema Minziro.

Kocha huyo aliyewahi kupita Yanga akiwa mchezaji na kocha, amesema maandalizi yao yanaenda vizuri,  akiamini kesho wataibuka na ushindi.


 
Geita imeanza kucheza Ligi Kuu msimu huu, lakini imeleta ushindani wa hali ya juu kwa timu mbalimbali inazokutana nazo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad