Makombora yapiga Kyiv, Umoja wa Mataifa wakiri kushindwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Makombora yamepiga Kyiv wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mjini humo, ambapo alikosoa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Antonio Guterres amesema baraza hilo limeshindwa kuzuia au kumaliza vita nchini Ukraine.

Hiki kilikuwa "chanzo cha kukatishwa tamaa sana, kufadhaika na hasira," alisema.

"Niseme wazi kabisa: [ilishindwa] kufanya kila kitu katika uwezo wake kuzuia na kumaliza vita hivi," aliongeza.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lenye wanachama 15 limepewa jukumu maalum la kuhakikisha amani na usalama wa kimataifa.

Lakini imekabiliwa na ukosoaji, ikiwa ni pamoja na serikali ya Ukraine, kwa kushindwa kuchukua hatua tangu uvamizi huo uanze mwezi Februari.


Urusi ni miongoni mwa wanachama watano wa kudumu wa baraza hilo na imepiga kura ya turufu zaidi ya azimio moja kuhusu mzozo huo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad