AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Maafisa wa idara ya ulinzi ya Marekani wamesema kuwa hatua ya Urusi kujiondoa katika mikoa ya Kyiv na Chernihiv sasa imekamilika.
“Vikosi vya Urusi karibu na Kyiv na Chernihiv vimekamilisha kujiondoa katika eneo hilo ili kuungana tena na kurejea Belarus na Urusi,” afisa wa Pentagon aliwaambia waandishi wa habari Jumatano.
“Hatuonyeshi vikosi vya Urusi ndani au karibu na Kyiv au ndani au karibu na Chernihiv,” msemaji wa Pentagon John Kirby baadaye aliongeza, akisema kwamba Rais wa Urusi Vladimir Putin “amefikia sifuri ya malengo yake ya kimkakati”.
“Kwa kweli anadhibiti tu vituo vidogo vya watu …. Hawajachukua Kharkiv.”
Inakuja siku chache baada ya Urusi kutangaza kwamba itaelekeza nguvu zake katika eneo la Donbas mashariki mwa Ukraine.
Afisa mkuu wa Pentagon, akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, alisema kwamba wanajeshi wa Urusi wanaweza kurudi Kyiv katika siku zijazo, na kwamba bado haijafahamika ikiwa wanajeshi wanaorejea ndio watakaotumwa tena
Kulingana na Taasisi ya Utafiti wa Vita ,vitengo vya Urusi vinavyorudi kutoka karibu na Kyiv vina uwezekano wa “kupata tena ufanisi wa vita kwa muda”.
Kati ya vikosi 130 vya Urusi ambavyo vimetumwa Ukraine, zaidi ya 80 bado vimesalia nchini, afisa huyo alisema.
Shirika la habari la Associated Press, likimnukuu afisa wa ulinzi wa Marekani, akisema kwamba idadi ya wanajeshi wa Urusi walioondoka ni takriban watu 24,000
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK