Aliyeiba Kanisani Aomba Kutubu kwa Mchungaji Kabla ya Kupelekwa Jela

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




John Kiiru, Mtuhumiwa
KIJANA mmoja aliyebainika kuiba vifaa vya muziki kwenye kanisa la Kenya Assemblies of God (KAG) mjini Eldoret nchini Kenya ameomba mahakama imruhusu akatubu.

John Kiiru mwenye umri wa miaka 18 aliyekiri kuiba vitu hivyo aliitaka

mahakama kumruhusu kuomba msamaha kutoka kwa uongozi wa kanisa hilo kabla ya kufungwa jela akidai pia kuwa anataka kukombolewa kabla ya kwenda jela.

Mshukiwa alimwambia hakimu wa mahakama ya Eldoret, Dennis Mikoyan, kuwa anataka kutumia kifungo chake gerezani kuwahubiria wafungwa wengine baada ya kugeuzwa kuwa ‘Kuzaliwa kwa mara ya pili katika Kristo’.

“Nimejutia sana nilichofanya, naomba mahakama hii inisaidie kumfikia pasta wa kanisa na viongozi wengine kuomba msamaha kabla ya kuhukumiwa,” aliiambia mahakama wakati akihukumiwa.

Hukumu ya kesi hiyo iliyovuta hisia ya watu wengi nchini humo inatarajiwa kutolewa mahakamani mnamo Juni 27, 2022.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad