Kilimanjaro: Mwanamke auawa na tembo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Saumu Hassan mwenye umri wa miaka 32, amefariki dunia baada ya kukanyagwa na tembo akiwa shambani katika kitongoji cha kijiweni wilayani Siha mkoani Kilimanjaro.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kilimanjaro Simon Maigwa amesema tukio hilo lilitokea farehe 19 mwezi huu majira ya asubuhi wakati mwanamke huyo akiwa shambani akichimba viazi.

Amesema mwanamke huyo alikutwa amefariki dunia baada ya kujeruhiwa na tembo, ambapo alipata majeraha makubwa kwenye mwili wake.

Kufuatia tukio hilo Kamanda Maigwa ametoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari pindi wanapokwenda shambani, hasa wale ambao wamepakana na hifadhi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad