Rais Samia kuhudhuria Tamasha hili, RC aomba Wananchi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye Tamasha la Utamaduni la kwanza kitaifa na Siku ya Kiswahili Duniani linalotaraji kuanza July 01-07 Jijini humo na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.


Akizungumza na Waandishi wa habari, RC Makalla amesema Tamasha Hilo litazinduliwa Julai 02 na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kwenye Uwanja wa Uhuru likihusisha Matembezi ya Utamaduni, Maonyesho ya vyakula vya asili na ngoma za asili.

Aidha RC Makalla amesema Julai 03 kutakuwa na Usiku wa Taarabu katika ufukwe wa Coco Beach ukihusisha burudani ya Mziki mwanana kutoka kwa wasanii mbalimbali akiwemo Khadija Kopa, Isha Mashauzi, Patricia Hilary, Mzee Yusuph na wasanii na vikundi ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson.


Hata hivyo RC Makalla amesema Julai 04 Kutakuwa na maandamano ya Amani kuhusu Lugha ya Kiswahili na Utoaji haki kutoka Temeke mwisho mpaka Uwanja wa Uhuru ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Katiba na sheria Dkt. Damas Ndumbaro.


 
RC Makalla amesema Julai 06 kutakuwa na kongamano la mchango wa lugha ya Kiswahili katika harakati za ukombozi wa bara la Afrika likihusisha Viongozi kutoka ndani na nje ya Nchi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad