Zari Amzidi Kibenteni Wake Miaka 25, Wafuasi Wake Wampinga, Awajibu Kuwa…

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Mwanamama tajiri Afrika Mashariki, raia wa Uganda mwenye maskani yake Durban nchini, Zari akiwa akiwa na mpenzi wake.
Zari The Boss Lady; ni mwanamama tajiri Afrika Mashariki, raia wa Uganda mwenye maskani yake Durban nchini Afrika Kusini na baby mama wa staa wa muziki wa Tanzania, Diamond Platnumz.

Zari ambaye amezaa watoto wawili na Diamond au Mondi, kwa sasa ana mpenzi mpya ambaye ni mdogo mno kiumri almaarfu kibenteni.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya burudani nchini Uganda, Zari mwenye umri wa miaka 41 (amezaliwa Septemba 23, 1980) anatoka kimapenzi na mvulana ambaye yeye (Zari) amemzidi kwa zaidi ya miaka 25.

Inasemekana mvulana huyo ni mkubwa kuliko mtoto wa kwanza wa Zari ambaye ni Pinto Ssemwanga.


 
Baadhi ya wafuasi wa Zari kwenye ukurasa wake wa Instagram waliojaribu kupingana na maamuzi yake hayo ya kutembea na watoto wenye umri sawa na watoto wake wa kuwazaa, Zari aliwajibu kuwa yuko tayari kutembea na mtoto mwenye umri sawa na mtoto wake wa mwisho ilimradi tu awe na uwezo wa kukidhi haja zake za kimahusiano.

Kumbuka kuwa mtoto wa Zari wa mwisho kwa sasa ni Prince Nillan ambaye hajafikisha hata umri wa miaka kumi hivyo ishu hiyo imeibua mjadala kama wote.

Zari amekuwa na mwanaume huyo miezi kadhaa baada ya kutengana na kibenteni mwingine aliyetambulika kwa jina GK Chopa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad