Mkenya Afariki Dunia Saudi Arabia Baada ya Mwajiri Wake Kumtoa Figo kwa Lazima

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Marehemu Rose Atieno aliwasili nchini Saudi Arabia mnamo Mei 23, 2022, na aliripotiwa kufariki dunia Juni 7.

Kulingana na mumewe marehemu, Abdulrazik Juma, alidai kuwa mke wake Rose Atieno alipiga simu kumfahamisha kuwa mwajiri wake alimlazimisha kufanyiwa upasuaji wa kutoa moja ya figo yake ambayo ingetolewa kwa mmoja wa jamaa yao aliyekuwa akiugua.

Mama Asimulia Kanisani Jinsi Alivyomuumbua Mke wa Zamani wa Mumewe: "Nilitandika Yeye"
"Sikuweza kumpata kwa zaidi ya siku tatu. Simu yake ilikuwa imezimwa na siku tano baadaye, alinipigia kwa namba tofauti na kuniambia kuwa ametekwa nyara na amelazwa katika hospitali ya mtaa kinyume na matakwa yake kutoa figo yake," alisema.


 
K24 inaripoti kuwa Juma hakuweza kuwasiliana tena na mke wake na baadaye, ni rafiki yake ndiye alimfahamisha kuwa aliaga dunia katika hospitali ambako alikimbizwa baada ya kudaiwa kuanguka kutoka kwa ngazi akisafisha madirisha nyumbani kwa mwajiri wake.

Mumewe mwendazake aliongeza kuwa mwili wa Ateno uliwasili nchini Jumanne, Julai 26, usiku kupitia kwa Uwanje wa Ndege wa Moi na ulipokelewa na familia.

“Mwili ulipowasili nchini na kupelekwa nyumbani kwa mkesha wa usiku nilipata muda wa kumuomboleza mke wangu na kumtazama kwa karibu mwili wake na kukuta alama za upasuaji tumboni mwake zinathibitisha vya kutosha kuwa alifanyiwa upasuaji kabla ya kufariki katika mazingira yasiyoeleweka," aliongeza.


Ajali ya Modern Coast Mto Nithi: Mke wa Dereva Asema Mumewe Alilalamika Sana Kuhusu Gari Bovu
Mganda atolewa figo bila kujua Saudi Arabia
Katika kisa sawia, Katika tukio tofauti, Judith Nakintu aliondoka kwenda Saudi Arabia mnamo 2019, lakini miezi kadhaa baadaye, alipoteza mawasiliano na familia yake, ambayo baadaye iliarifiwa kwamba alikuwa amehusika katika ajali.

Nakintu alirejea nyumbani hivi majuzi, na kwa mshtuko wa familia yake, walifadhaika sana kumuona kwenye kiti cha magurudumu na kuhangaika kuongea kwa sababu ya kupooza.

Walimpeleka kwa uchunguzi wa kimatibabu baada ya kuwasili, na madaktari waligundua kuwa figo yake ya kulia ilikuwa imetolewa bila kujua au idhini yake.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad