Kumekucha..Mahakama ya Juu Yakataa Maombi Mawili ya William Ruto Katika Kesi ya Kupinga Ushindi Wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Ombi la Rais Mteule William Ruto la kutaka ushahidi wa makamishna sita wa IEBC kutupiliwa mbali limekataliwa
Katika ushahidi aliowasilisha mahakamani, Ruto aliteta kuwa uchaguzi wa Agosti 9, uliendeshwa na IEBC na wala sio makamishna binafsi
Ombi lake pia la kutaka Chama cha Mawakili Nchini (LSK) kuzuiliwa kushiriki katika kesi hiyo pia limekataliwa
Mahakama ya Upeo imekataa maombi matatu kuelekea kikao cha leo Jumanne, Agosti 30, kuweka kanuni za kuiendesha kesi ya kupinga matokeo ya urais ya uchaguzi wa Agosti 9.

Ombi la Rais Mteule William Ruto la kutaka ushahidi wa makamishna sita wa IEBC kutupiliwa mbali limekataliwa
Ombi la Rais Mteule William Ruto la kutaka ushahidi wa makamishna sita wa IEBC kutupiliwa mbali limekataliwa. William Ruto.
Maombi hayo ni pamoja na ya Rais Mteule William Ruto ambaye alikuwa anataka Chama cha Mawakili Nchini (LSK) kuzuiliwa kushiriki katika kesi hiyo.

Ruto alihoji kuwa LSK haitakanin kushirikishwa katika kesi hiyo kwa sababu Martha Karua, ambaye ni mlalamishi, ni mwanachama wake na pia kiongozi wa zamani.

LSK kilikuwa kimewasilisha ombi la kushirikishwa katika kesi hiyo kama mshauri wa korti kikisema kina utaalam wa kusaidia Mahakama ya Juu kufikia uamuzi wa haki.


Mwaure Akimbia Mahakamani Kutetea Ushindi wa Ruto: "Yuarona, It Was Free and Fair
Vile vile ombi la Ruto la kutaka ushahidi wa makamishna sita wa IEBC kutupiliwa mbali pia limekataliwa.

Katika ushahidi aliowasilisha mahakamani, Ruto aliteta kuwa uchaguzi wa Agosti 9, uliendeshwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) na wala sio makamishna binafsi.

Makamishna hao ni Juliana Cherera, Francis Wanderi, Irene Masit, Justus Nyang'aya, Boya Molu na Abdi Guliye.


Kupitia wakili wake Kithure Kindiki, Ruto alisema kuwa makamishna hao sita walishtakiwa kimakosa na kwamba pia wana uhasama na mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati.

Alidai kuwa ushahidi wa makamishna hao utayumbisha ushahidi wa Ruto kwa sababu ya kuumbua madai mapya na lawama dhidi yake.

Mahakama ya Juu pia imetupilia mbali ombi la Chama cha Agano la kutaka kushirikishwa katika kesi hiyo.

Agano kilikuwa kikijaribu kupinga kesi ya Azimio dhidi ya tangazo la IEBC ambalo William Ruto alitangazwa kuwa rais mteule.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad