Wanne wadaiwa kufa moto mganga akiwaondolea mikosi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




WATOTO wanne wamefariki dunia baada ya kuungua na wengine saba kujeruhiwa kwa moto uliowashwa kwa madai ya kuondoa mkosi katika familia.

Vifo hivyo vilitokea usiku wa kuamkia jumatano katika Kijiji cha Magili Juu, Kata ya Kigwa wilayani Uyui mkoani Tabora na moto huo unasadikiwa kuwa uliwashwa na mganga aliyekuwa amekwenda kuwaondolea mkosi.

Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Tabora, Richard Abwao alithibitisha tukio hilo na kusema mganga anayetuhumiwa kuhusika amekamatwa na kwamba upelelezi wa tukio hilo unaendelea.

Akieleza undani wa tukio hilo, Diwani wa Kata ya Kigwa, Bakari Kabata alieleza kuwa mkuu wa kaya alimuita mganga wa kienyeji kwenda kuondoa mkosi kwenye familia hiyo.


Kwa mujibu wa Kabata, mganga aliagiza kitengenezwe kibanda cha nyasi na kuwaambia waingie ndani ili akiwashe moto na wao watoke nje mmoja baada ya mwingine.

Alisema moto huo ulizidi kisha kusababisha watu hao wanne kupoteza maisha.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Magili Juu, Said Magari alitaja waliofariki kuwa ni Kashindye Machia (5), Shija Samwel (5), Dotto Masasi (3) na Jeremia Samwel (7).


Waliojeruhiwa ni Samwel Masasi (40), Sida Samwel (10), Masasi Samwel na Dotto Machia (wote miaka 9), Shija Samwel miaka (7), Halima Samwel (11) na Regina Masanja (65).
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad