Mapacha Waoa na Kumpachika Mimba Mke Mmoja: "Tunalala Kitanda Kimoja"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kaka mapacha, Teddy na Peter wako katika uhusiano wa mapenzi na mwanamke mmoja kwa jina Emily ambaye wanadai ni mke wao
Uhusiano huo wa kushangaza umempelekea Emily kupata mimba na amefichua kuwa hafahamu ni nani kati ya mapacha hao ndiye baba halisi wa mwanaye
Emily, Teddy na Peter walisimulia kuwa walikutana katika hafla ya kanisa na kuanza kuchumbiana baada ya kubadilishana nambari za simu
Mapacha wawili wamezua mjadala mtandaoni baada ya kufichua kuwa wamemuoa mke mmoja na wanatarajia kupata mtoto hivi karibuni.

Mapacha Wakorino Waoa na Kumpachika Mimba Mke Mmoja: "Tunalala Kitandani Kimoja"
Mapacha Wakorino Waoa na Kumpachika Mimba Mke Mmoja. Picha: Nicholas Kioko.
Watatu hao wakiwa wamevalia kofia za Akorino na mashati yanayofanana, waliwaacha wengi vinywa wazi baada ya kufichua kuwa wanalala kitanda kimoja.

Katika video kwenye Youtube iliyopakiwa na mwanablogu Nicholas Kioko, watatu hao walisema wanapendana sana.

Mapacha hao, Teddy na Peter walidai kuwa hawajafunga ndoa rasmi na Emily ingawa wanaishi nyumba moja na hivi karibuni wanatarajia kuitwa baba.


William Ruto Awaonya Cartels, Asema Atawakabili Vilivyo
"Sisi ni familia, huyu ni mke wetu, mimi na kaka sisi ni mapacha. Tuna mke mmoja kwa sababu sisi ni mapacha," alisema Teddy.

Aliongeza kuwa:

"Tunaishi pamoja, tunalala kitanda kimoja. Sisi ni watu na bibi yao. Sisi ni mapacha. Kuna hii kitu mapacha hukuwa nayo, mmoja akipenda pia huyo mwingine anapenda."

Emily kwa upande wake alisema: "Wote wawili ni mabwana zangu. Nawapenda wote wawili."

Mrembo huyo alifichua kuwa walikutana katika ibada ya kanisa na kubadilishana nambari za simu na Peter ambaye wakati huo hakuwa na simu, alikuwa akitumia ya kaka yake.

Wakati alipoulizwa ni nani aliyempachika mimba, Emily alisema:

"Mimba sijui ni ya nani. Tunashare the same bed, kila kitu ni kimoja sasa siwezi jua kama ni ya huyu ama huyu."

Peter alisema baada ya kuwapasha habari za ujauzito wake walikubali kuwajibika kwa sababu wapo kwenye uhusiano wa kweli.


Oparanya Asema Wanasiasa Wanaokimbilia Kenya Kwanza ni wa Bei ya Chini: " Too Cheap"
"Tuko serious na yeye na tuko na future na yeye," alisema.

Katika hadithi tofauti, TUKO.co.ke iliripotia kuhusu mapacha watatu ambao walifichua kwamba wako katika uhusiano wa mapenzi na mwanamume mmoja aliyependana nao nyakati tofauti.

Eve, Mary na Cate walisema wamefurahishwa sana na kuchumbiana na mwanaume mmoja kwa sababu anawapa mapenzi na muda sawa.

Warembo hao walisema wamekuwa wakichumbiana na mwanamume huyo kwa mwaka mmoja na nusu sasa na wanapanga kuoana.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad