RASMI Mo Simba Arena kuzunguushiwa ukuta

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla leo Jumatano (Septemba 14) amemaliza mgogoro wa Ardhi katika kiwanja namba 229 Kinachomilikiwa na Simba SC maeneo ya Bunju B Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

RC Makalla baada ya kuzuru eneo la kiwanja alipata wasaa wa kujionea mipaka na Wananchi takribani 9 ambao wamevamia na kujenga katika eneo hilo.

Aidha RC Makalla amewataka wananchi waliovamia katika kiwanja hicho ndani ya siku 60 kuanzia leo Jumatano (Septemba 14) kujipanga kuondoka mara moja kwa kuwa eneo hilo ni mali halali ya Simba SC ndio wenye hati miliki.

“Uvamizi wa Ardhi ni ualifu kama ulivyo ualifu mwingine wowote ambapo anayetenda kosa anastahili kuchuliwa hatua za kisheria” Amesema RC Makalla


RC Makala walipokua akikagua sehemu ya eneo la Uwanja wa Simba Bunju B, Dar es salaam
Katika hatua nyingine RC Makalla ameelekeza Uongozi wa Simba SC kuanza mara moja ujenzi wa uzio kuzunguka kiwanja hicho kama walivyokusudia huku akimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe amemuagiza OCD kusimamia Ulinzi na Usalama katika eneo hilo katika Kipindi chote cha Utekelezaji wa zoezi hilo.

Hata hivyo RC Makalla ametoa Rai kwa Simba SC kuendeleza uwekezaji wa kiwanja hicho kwa kuwa ni fursa ya kibiashara kwa wakazi wa Bunju Wilaya, Mkoa na Taifa kwa Ujumla.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad