Wamaasai 8 Waliomshambulia Askari Jela Miezi Sita

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Vijana 8 wa jamii ya kifugaji ya Maasai, Kiteto mkoani Manyara, waliomshambulia kwa marungu Askari wa Jeshi la Polisi Kata ya Njoro, Inspekta Patrick, wamehukumiwa kwenda jela miezi sita ama kulipa faini ya shilingi elfu 50 na fidia ya laki 1 kwa kila mmoja.


Vijana walikuwa wanashtakiwa kwa makosa mawili, ambapo kosa la kwanza ni kumshambulia Askari Polisi wa Kata ya Njoro A/ Inspekta Patrick aliyeitwa kusaidia kuondoa mifugo iliyokuwa inakula mazao shambani, na shtaka la pili ni kumpiga Askari Mgambo waliokuwa na Askari huyo katika tukio hilo.


Hakimu wa Mahakama ya wilaya ya Kiteto, Boniface Lihamwike, alipowauliza watuhumiwa hao kuhusu madai ya makosa hayo mawili, watuhumiwa walikiri makosa kuwa waliyatenda wao wenyewe.


Mwendesha mashtaka Salimu Issa Bakari aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Alangai Manywele, Elenyoki Manywele, Lazaro Mbuki, Kamunga Mbuki, Mteriani Mbuki, Mukara Ngurdada, Moita Taleck na Kilesii Alli


Hakimu Boniphasi Lihamwike Aliwauliza watuhumiwa kama wana cha kujitetea ambapo waliiomba Mahakama iwapunguzie adhabu huku wakisema kuwa hilo ndio kosa lao la kwanza na pia wanategemewa na familia.


Hata hivyo washtakiwa hao kwa pamoja walilipa faini hiyo.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad