Rais Samia Awakanya Wanaosubiri Mkeka wa Uteuzi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wakuu wa wilaya kufanya kazi kwa weledi na kuacha kusubiri mkeka wa uteuzi na kuwataka wakuu wa mikoa kusimamia utendaji kazi wa viongozi wa wilaya kwa kuwasilisha ripoti.


Rais Samia ameyasema hayo katika hafla ya utiaji saini Mkataba wa Usimamiaji wa Shughuli za Lishe leo Septemba 30, 2022 jijini Dodoma.


“Nasikia hamfanyi kazi mnasubiri mkeka napata mesage, malizia huku hawafanyi kazi wako kama wamepigwa ganzi. nikute mkuu wa wilaya kapigwa gazi, nikute kapigwa gazi! nilisema tulichokifanya ni performance ya utendaji wenu,” amesema Rais Samia.


“Sikusema nitawabadilisha leo na kesho nimesema tumefanya perfomance tumejua nani mzuri nani mbaya aliyesema nataka kuwabadilisha nani? kama wabaya nilitaka kuwatia kwenye mafunzo niwarekebishe, kwahiyo kama hamfanyi kazi hao ndio wangu,” amesema Rais Samia.


“Wakuu wa wilaya nchi nzima fanyeni kazi zenu, kutoa mkeka ni kazi yangu na nitatoa wakati ninapoona muafaka sasa hivi kwenu ni kufanya kazi,”


“Wakuu wa mikoa nataka ripoti za wakuu wenu wa wilaya aliyepigwa gazi nani, mwenye nusu kaputi nani kama hawawezi tutoe tuweke wengine nataka ripoti za wakuu wenu wa wilaya na hili tutalizungumza jioni leo,” ameongeza Rais Samia

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad