Watu Saba wa Familia Moja Wateketezwa na Moto Hadi Kuaga Dunia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA






Watu saba wa familia moja wameaga dunia kufuatia kisa cha moto kilichotokea usiku wa Ijumaa, Oktoba 1, katika kijiji cha Ngimari kaunti ya Embu.

Watu Saba wa Familia Moja Wateketezwa na Moto Hadi Kuaga Dunia
Picha ya maktaba ya nyumba inayoteketea.
Saba hao ni mwanamume mmoja, mkewe, binti zake wawili, mvulana mmoja na wajukuu wake wawili na waliangamia baada ya moto kuteketeza nyumba yao.

Kwa mujibu wa ripoti, saba hao walichomeka kwa kiasi cha miili yao kutotambulika huku nyumba yao inayoripotiwa kutengenezwa kwa mbao kuteketea kabisa.

Maafisa wa polisi kutoka Runyenjes wamefika eneo la tukio ambalo tayari limejaa wakaazi wa eneo hilo huku hali ya majonzi ikitawala kijiji hicho.

Chanzo cha moto huo bado hakijabainika. Kisa hicho kinajiri wiki moja baada ya nyumba nyingine kuteketea hadi kuwa majivu katika kijiji cha Gikuuri eneo bunge la Runyenjes.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad