Juma Mgunda: Kuna Kazi Kubwa ya Kufanya Simba SC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kaimu Kocha Mkuu wa Simba SC Juma Ramadhan Mgunda amesema hana budi kuanza kuisuka upya safu yake ya Ushambuliaji, ili irejee katika hali yake ya kawaida baada ya kusuasua kwenye michezo miwili ya Ligi Kuu Tanzania Bara.


Simba SC ilipata wakati mgumu ilipocheza ugenini Singida dhidi ya wenyeji wao Singida Big Stars na kuambulia sare ya 1-1, kisha ikashinda kwa mbinde dhidi ya Ihefu FC nyumbani Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.


Kwenye mchezo dhidi ya Singida Big Stars, Phiri alikosa nafasi ya kufunga dakika ya 7, 20, 44, 52 na 71 huku Kibu Dennis akikosa nafasi ya kufunga dakika ya 47, 51 na 66.


Benzema afunguka ya Cristiano Ronaldo

Mgunda amesema kuwa furaha ya Kocha ni kuona timu inapata matokeo mazuri ambayo ni ushindi pale inapokuwa tofauti huwa hakuna anayefurahia jambo hilo.


“Kweli wachezaji wanapambana kusaka ushindi na wanacheza pia tunatengeneza nafasi nyingi lakini ambazo tunatumia ni chache hivyo hilo tunalifanyia kazi kwa ajili ya kupata matokeo kwenye mechi zetu zote katika eneo la mazoezi,” amesema.


Safu ya ushambuliaji imetupia mabao 19 na kinara ni Moses Phiri mwenye mabao matano na pasi mbili za mabao.


Simba SC imeshajikusanyia alama 21 baada ya kucheza michezo 10, huku Young Africans ikiwa kileleni kwa kufikisha alama 23 baada ya kucheza michezo 9.


----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad