Kocha wa Timu ya Taifa ya Cameroon Rigobert Song Afafanua Kumtimua Andre Onana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kocha wa Timu ya Taifa ya Cameroon Rigobert Song amekanusha taarifa za kumtimua Mlinda Lango Andre Onana, kwa sababu za kukataa kutii amri ya kutimiza jukumu la ushirikiana na kupinga mpango wa Rais wa Shirikisho la Soka nchini humo Samuel Eto’o kufanya mazoezi ya timu hiyo.


Onana aliondolewa kwenye kikosi cha Cameroon saa chache kabla ya mchezo pili wa Kundi G dhidi ya Serbia uliomalizika kwa timu hizo kufungana 3-3.


ong amesema amelazimika kumuondoa Mlinda Lango huyo wa klabu ya Inter Milan ya Italia, kwa sababu za kinidhamu ambazo zilipelekea washindwe kuelewana, hasa alipokataa kucheza mchezo dhidi ya Serbia jana Jumatatu (Novemba 28).


“Ni mchezaji muhimu, lakini tuko kwenye michuano migumu, hivyo ni bora akatupisha ili tumalize hili kwanza,”


“Ninajua ninachopaswa kufanya, na hiyo ni kuhakikisha kuwa timu kwanza halafu mchezaji baadae.” alisema kocha huyo baada ya mchezo dhidi ya Serbia


Alipoulizwa na Shirika la Habari la AFP iwapo angeanza mchezo wa jana dhidi ya Serbia badala ya Onana, Mlinda Lango namba mbili Devis Epassy alijibu “Ningependa hili swali aulizwe Kocha Song, mimi sitakua tayari kujibu”


Ninachojua hakuna tatizo lolote katika kambi yetu hapa QATAR.” alisema Devis Epassy


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad