Meli Kubwa Inayodaiwa Kutaka Kuiba Mafuta ya Nigeria Yakamatwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Meli kubwa ya kubeba mafuta ambayo imeshutumiwa na serikali ya Nigeria kwa kujaribu kupakia mafuta ghafi kinyume cha sheria kabla ya kuondoka katika maji iya nchi hiyo, imelazimishwa kurudi ilipotoka.


Equitorial guinea iliikamata meli hiyo kwa jina Heroic Idun, kutokana na ombi la serikali ya Nigeria.


Idun ina uwezo wa kubeba mapipa milioni 2 ya mafuta, na ilikamatwa Agosti 17, kwa kusafiri bila bendera inayoitambulisha na hivyo ilikuwa vigumu kutambuliwa.


Ilikuwa inatokea katika maji ya Nigeria ikielekea Equitorial Guinea bila idhini.

 


Serikali ya Nigeria imesema kwamba meli hiyo inamilikiwa na kampuni ya Idun na msemaji wa jeshi la majini la Nigeria Commodore Kayode Ayo Vaughan, amesema kwamba meli mbili ndogo za jeshi la Nigeria, zinaisindikiza meli hiyo kurudi Nigeria.


Taarifa zinasema kwamba meli hiyo ilikuwa inaelekea Bonny, Nigeria. Makam rais wa Equitorial Guinea Teodoro Nguema Obiang, ameandika ujumbe wa twitter kwamba aliamuru meli hiyo kurudi Nigeria.

Nigeria hupoteza mapipa 400,000 ya mafuta kila siku kutokana na wizi.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad