Msafara wa Jeshi Washambuliwa, 14 Wafariki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Jumla ya watu 14 wamefariki dunia, baada ya kutokea kwa shambulizi la ghafla katika msafara wa kijeshi wa waasi, wanaoungwa mkono naSerikali ya Iran katika eneo la mashariki mwa Syria lililo karibu na mpaka wa nchi ya Iraq.


Kwa mujibu wa Shirika la Syrian Observatory for Human Rights, linalofuatilia haki za binadamu nchini Syria, lenye makao yake nchini Uingereza limesema shambulizi hilo limefanywa katika malori yaliyokuwa yamebeba mafuta na silaha eneo la Albu Kamal.


Kufuatia shambulio hilo, Muungano wa kijeshi unaoongozwa na vikosi vya kijeshi vya nchi ya Marekani umewaambia waandishi wa habari kwamba hauhusiki na shambulizi hilo.


Hata hivyo, Afisa mmoja wa ulinzi wa Irak amesema malori hayo yalikuwa yanasafirisha mafuta kutoka Iran kuelekea Lebanon, kupitia Irak na Syria ukijumuisha malori 22 ambapo 10 kati ya hayo yalishambuliwa baada ya kuingia Syria.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad