Mwamba Amuibia Mpenzi Wake Mamilioni na Kumuhonga Mchepuko

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanaume mmoja jijini Nairobi nchini Kenya amepandishwa kizimbani kwa madai ya kuiba viatu na kompyuta mpakato ya mpenzi wake yenye thamani ya Ksh.25,000 (TZS 474,197) kisha kumpa mpenzi wake mwingine.

Ryan Lusalishi alifikishwa mbele ya Mahakama ya Sheria ya Makadara siku ya Alhamisi, ambapo mahakama imedai mshtakiwa aliiba kompyuta mpakato, begi na jozi ya viatu vya Elizabeth Okumu kati ya Novemba 7 na 8 mwaka huu jijini Nairobi.

Kulingana na Bi. Okumu ambaye alitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkuu, Gathogo Sogomo amedai aliporejea nyumbani kwake alikuta baadhi ya vitu vimepangwa upya, na wakati alipokagua ndipo aligundua kuwa kompyuta ndogo, jozi ya viatu, begi na kadi ya ATM hazikuwepo.

Okumu ameiambia mahakama kuwa siku hiyohiyo, alipokea ujumbe wa muamala uliofeli wa PIN isiyo sahihi uliompa mashaka kuwa kuna mtu alikuwa akijaribu kutumia kadi yake ya ATM ambayo imeibwa na baada ya kujithibithishia kuwa hakuna mtu mwingine aliyeingia nyumbani alishuku kuwa ni mpenzi wake na kupiga simu polisi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad