Serikali Yatoa Tamko Suala la Ushoga Mashuleni...

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Na Dotto Kwilasa,DODOMA.


SERIKALI imesema inafuatilia kwa karibu taarifa zilizotolewa hivi karibuni na vyombo vya habari kuhusu shule ambazo zinafundisha wanafunzi masuala ya ushoga jambo ambalo ni kinyume na mitaala ya elimu hapa nchini.



Hatua hiyo imekuja kufuatia hivi karibuni chombo kimoja cha habari nchini kuripoti tukio la wanafunzi kulawitiana mkoani Kilimanjaro kinyume na taratibu za elimu zinavyotaka na kwenda kinyume na mila na desturi za Mtanzania.


Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma Waziri wa elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema kutokana na hali hiyo tayari Serikali imewapeleka Kamishina wa Elimu, Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora pamoja na Mwanasheria wa Wizara kufuatilia jambo hilo ili kuwabaini waliohusika.


"Kwa sasa hivi timu hiyo inapitia hizo shule na kupata taarifa lakini pia tumemuomba mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kushirikiana na timu hiyo pamoja na kuwasaidia sehemu ambayo ina masuala jinai ili polisi wachukue hatua,"amesema.



“Tunatarajia kwamba hao walioenda wataleta taarifa kamili na sisi tuko tayari kuchukua hatua stahiki kudhibiti mambo hayo, zaidi ya hayo kwa kuwa suala hili limetokea eneo moja basi tunajua kunaweza kukawa na taarifa kwenye maeneo mengine,"amesisitiza


Pamoja na hayo Waziri huyo mwenye dhamana ya elimu nchini amesema kupitia wizara hiyo Katibu Mkuu atatoa namba ambayo mtu yeyote mwenye taarifa kama hiyo katika shule yeyote iwe ya umma au binafsi au vyuo vyovyote hapa nchini aweze kuwasiliana naye moja kwa moja .



“Tutafuatilia kwa nchi nzima, tunaongeza umakini kwa kufuatilia mambo haya kwa sababu tunajua yanaweza kuchafua taswira ya elimu,yanaharibu vijana wetu na hata wazazi kukosa imani na shule”, amesema.


Kwa kutilia mkazo suala hilo, Prof. Mkenda amesema walifanya mkutano ambao ulikuwa chini ya Mwenyekiti Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu George Simbachawene,Waziri wa Maendeleo ya jamii Dk. Dorothy Gwajima na Waziri wa TAMISEMI pamoja na makatibu wakuu kwa ajili ya kuangalia namna ya kudhibiti mambo hayo.


“Suala hili ni nyeti na lazima tulishughulikie kwa umakini mkubwa,tumeanza mkakati wa kitaifa wa kuangalia namna ya kudhibiti tatizo hili kuanzia majumbani, njiani na maeneo mbalimbali ,"amesema.


----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad