AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hali mbaya ya usalama kusini mwa Uturuki imevuruga juhudi za uokoaji kufuatia tetemeko baya la ardhi lililotokea Jumatatu, makundi ya kimataifa yamesema.
Wafanyakazi wa uokozi wa Ujerumani na jeshi la Austria walisitisha shughuli zao za utafutaji, wakitaja mapigano kati ya makundi ambayo hayakutajwa.
Pia kumekuwa na ripoti za uporaji. Rais wa Uturuki amesema atatumia mamlaka ya dharura kumuadhibu yeyote atakayevunja sheria.
Idadi ya vifo kutokana na tetemeko la ardhi sasa imepindukia 25,000 na matumaini yanafifia ya kupata manusura wengi zaidi chini ya vifusi, licha ya visa vya uokoaji wa miujiza.
Kulikuwa na ripoti mapema Jumamosi kwamba mapigano kati ya makundi yasiyojulikana katika jimbo la Hatay yamewaacha wafanyakazi kadhaa kutoka Kitengo cha Misaada ya Maafa cha Vikosi vya Austria wakitafuta hifadhi katika kambi ya msingi na mashirika mengine ya kimataifa.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK