Daktari: Mtu Mmoja Anatakiwa Kufanya Ngono Mara Tatu kwa wiki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Daktari: Mtu Mmoja Anatakiwa Kufanya Ngono Mara Tatu kwa wiki


Wanaume wanaopenda kufanya ngono mara kwa mara wanadaiwa kuwa kwenye hatari ya kufariki mapema tofauti na wanaume ambao hawafanyi kitendo hicho mara kwa mara.

Hayo yamesemwa na daktari bingwa wa afya ya uzazi kutoka Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar, Dkt. Ummukulthum Omar wakati akitoa mafunzo ya afya ya uzazi kwa wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika eneo la Tunguu, Zanzibar.

Dkt. Omar amebainisha kuwa wanaume wanaopenda kufanya ngono hufariki dunia mapema kwa sababu hutumia nguvu nyingi wanapofanya tendo la hilo, hali inayowasababisha kuishiwa nguvu kwenye miili yao.

Aidha, amesema kitaalamu mtu mmoja anatakiwa kufanya tendo la ndoa mara tatu ndani ya wiki moja ili kuuweka mwili sawa na kwamba anapofanya zaidi ya inavyoelekezwa hujiweka katika hatari.

“Kufanya tendo la ndoa kila siku kunahatarisha afya ya mwili, hivyo ni vyema wanandoa kufanya kitendo hicho kwa kufuata utaalamu kutoka kwa wataalam wa afya na isiwe mnafanya jambo hilo kwa kukomoana,” ametahadharisha Dkt. Omar


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad