Jeshi la Polisi "Tunamchunguza na Kumfanyia Vipimo Askari Aliyefanya Vitendo vya Ushoga"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jeshi la Polisi "Tunamchunguza na Kumfanyia Vipimo Askari Aliyefanya Vitendo vya Ushoga"

Jeshi la Polisi Zanzibar limesema linamchunguza askari anayetuhumiwa kujiuhusisha na mapenzi ya jinsia moja (ushoga) na kwamba endapo ikithibitika kuna ukweli wa jambo hilo, atafikishwa mahakamani pamoja na kufukuzwa kazi.


Hayo yameelezwa na Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamad Khamisi Hamad wakati akizungumza na Nipashe akibainisha kuwa ofisi yake ina mpango maalum wa kuwasaka askari wake wote wenye hulka na kujihusisha na matendo ya aina hiyo.


“Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kadhia hiyo ikiwemo kufanyiwa kipimo askari huyo ili kujidhihirisha kama kweli anafanya kitendo hicho. Ingawa tumeona video katika mitandao ya kijamii lakini hatuwezi kusema moja kwa moja kama ni kweli au siyo kweli,” amesema.


Aidha, Kamishna Hamad amesema askari anapojihusisha na mapenzi ya jinsia moja hukosa uaminifu na ukakamavu katika jukumu lake la msingi la kulinda raia na mali zake na kuongeza kuwa ni kinyume na tamaduni za nchi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad