Mama Samia Aongeza Dau Mabao Kimataifa sasa Kila Goli Milioni 10

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Awali Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan aliahidi kuizawadia timu ya Taifa 'Taifa Stars' Tsh Milioni 500 kama itafanikiwa kufuzu fainali za michuano ya Afcon 2023 zitakazofanyika huko Ivory Coast

Jana baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Uganda katika mchezo uliopigwa huko Misri, Rais Samia ameongeza bonas kwa Stars

Katika michezo mitatu iliyobaki, Stars itavuna Tsh Milioni 10 kwa kila bao watakalofunga

Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa amesema kuanzia mchezo wa marudiano dhidi ya Uganda ambao utapigwa Jumanne, Tsh Milioni 10 zitaanza kutolewa kwa kila bao la Stars

Rais Samia anatoa Tsh Milioni 5 kwa timu za Simba na Yanga kwa kila bao wanalofunga kwenye michuano ya ligi ya mabingwa na kombe la Shirikisho barani Afrika

Takribani Tsh Milioni 85 zimetolewa katika mechi tano za hatua ya makundi ambazo Simba na Yanga wamecheza mpaka sasa

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad