Askari Polisi adaiwa kumbaka mwanafunzi aliyekuwa mahabusu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Kenya. Mwanafunzi wa kidato cha kwanza aliyekuwa akishikiliwa katika kituo cha polisi cha Khwisero kilichopo Kaunti ya Kakamega nchini Kenya anadaiwa kubakwa na mmoja wa ofisa wa polisi wa kituo hicho.

Kwa mujibu wa tovuti ya Tuko ya nchini humo imesema mwanafunzi huyo alikamatwa Aprili 28, mwaka huu akiwa na rafiki yake kwa kosa la kwenda kwa mtu anayesemekana ni mpenzi wake, hivyo wazazi wao wakawaomba polisi kuwakamata na kuwasweka mahabusu kama adhabu.

Wakiwa kituoni hapo askari alikwenda na kumtaka mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 16, kumfuata kwenye chumba kingine ambapo alimuamuru avue nguo.

Mkurugenzi wa Huduma za Kijamii, Huduma za Watoto, Utamaduni na Jinsia wa kaunti hiyo, Vivian Ayuma amesema kuwa mtuhumiwa alimnajisi mtoto huyo kwa kutumia kinga (kondomu) ingawa bado hajakamatwa. 


"Hili ni jambo la kusikitisha sana ambalo limefunikwa chini ya kapeti. Tunaomba uchunguzi kamili ufanyike kuhusu tukio hili la kusikitisha. Tunahitaji askari huyu afunguliwe mashtaka kwa kumsababishia binti maumivu na kuharibu maisha yake," amesema Ayuma.

Imeandaliwa na Sute Kamwelwe.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad