Askari wa JWTZ ampiga na kumjeruhi dereva wa basi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Tukio hilo linaelezwa kutokea juzi majira ya saa 1:30 asubuhi katika eneo la Kibaha Kwa Mathias baada ya Shabani (45) aliyekuwa akiendesha basi la Saratoga lenye namba za usajili T 555 DCZ kushambuliwa na kupigwa na askari huyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi (ACP) Pius Lutumo, alithibitisha jana kutokea kwa tukio hilo. Alisema mtuhumiwa ambaye ni askari wa JWTZ, Koplo Emmanuel Peleka, alimshambulia dereva huyo na kumsababishia kushindwa kuendelea a safari.

Kwa mujibu wa NIPASHE, Kamanda Lutumo alisema kutokana na tukio hilo, Shabani alilazimika kwenda kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufani ya Tumbi.

Lutumo alisema chanzo cha tukio hilo ni Koplo Peleka ambaye ni dereva wa gari la jeshi, kujaribu kulipita basi la Saratoga na kuwekewa pingamizi, jambo ambalo lingesababisha ajali, hivyo kusababisha taharuki iliyosababisha gomvi baina yao.

Kamanda Lutumo alibainisha kuwa tayari hatua za kisheria zimechukuliwa kwa kumhoji mtuhumiwa na kupata maelezo ya mwathirika.

Kutokana na tukio hilo, Lutumo alitoa wito kwa madereva kutii sheria za usalama barabarani ili kuepusha taharuki na ajali zinazoweza kusababisha madhara na kusisitiza kuwa mbele ya sheria, wote wako sawa na hakuna aliye juu ya sheria.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad