Faiza Ally Awashukia Wanaomsema Paula Kajala " Huyu Binti ni Mtu Mzima Ana Miaka 18 Mwacheni"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Faiza Ally Awashukia Wanaomsema Paula Kajala " Huyu Binti ni Mtu Mzima Ana Miaka 18 Mwacheni"


Msanii wa Bongo Movies na mjasiriamali, Faiza Ally amesema kuwa mwanaye Sasha si sawa na Poaula wa Kajala kwani kila mtu amezaliwa na kuishi kwa namna yake kulingana na mipango ya Mungu.


Faiza amesema wanaomsema Paula na mama yake Kajala wanakosea kwani binti huyo na ni mtu mzima ambaye anayo haki ya kuamua jambo lolote hata mahusiano bila kulazimishwa na mtu.


"Hili swali huwa naulizwa mara nyingi sana kwamba je ningependa mwanangu awe kama Paula? Nikicheza na Mwanangu naambiwa namtengeneza Paula, najibu kwa pamoja, Paula na Sasha ni binadamu wawili tofauti, kwa imani yangu kila binadamu ana stori yake iliandikiwa.


"Ukiniuliza kuhusu Paula nitakwambia ni binti wa kawaida kama wengine wote, Paula ni msichana wa zaidi ya miaka 18 ana haki na uhuru wa kuwa na anaemtaka.


"Zamani wazazi wetu waliolewa kuanzia miaka 10 na zaidi, mtaani watoto kama Paula wana watoto na mabwana wa kutosha, Paula amebahatika kuwa Star na siyo tu kuzaliwa na Star kwasababu wazazi wake ni Mastaa hivyo habari yake ya bwana ni habari ya kitaifa.


"Kiufupi Khan (Mtangazaji wa Clouds Media) ni mzalilishaji kwa njia ya maneno, Paula hana ajabu katika anayoyafanya ajabu inakuwa ajabu kwenye macho yenu kwasababu mnaona na picha, lakini huko mtaani mnafanya makubwa zaidi ya Paula.


"Paula mwanangu, kuwa jasiri mama wewe ni Star siyo mtu yoyote, kweli kuna wakati nilichukizwa juu ya mapenzi yangu kwa Fahyma lakini haya yamepita mimi ni mmoja kati ya watu wanao mpenda sana Fahyma, na familia yake na sasa nimefurahi sana wako pamoja Alhamdulillah wadumu.


"Na wewe utapata njia yako, bado ni msichana mdogo mzuri dunia yako binti yangu najua uko kwenye age ya moto sana, utapatwa na mengi mno, tumia akili zaidi utafika mbali, hawa wanaokuona unakosea leo kesho watakupigia makofi, kuna siku, stay strong and focus," amesema Faiza.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad