Paula akabiliana vikali na mama yake Kajala baada ya Rayvanny kumtembelea kisiri

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Paula alikuwa amemleta Rayvanny katika kikao kilichokusudiwa kwa familia tu, jambo ambalo liliamsha hasira za Kajala.
Muhtasari
•Wawili hao walikabiliana kwa maneno baada ya Paula kumwalika Rayvanny kwenye kikao cha kambi ambacho kilikusudiwa kuwa cha familia tu.

•Paula alimjibu mamake kwa kumkumbusha kuwa pia yeye ana maisha yake na kuwa hakuwahi kumhoji alipokwenda kwa Harmonize.

•Wawili hao walikabiliana kwa maneno baada ya Paula kumwalika Rayvanny kwenye kikao cha kambi ambacho kilikusudiwa kuwa cha familia tu.

•Paula alimjibu mamake kwa kumkumbusha kuwa pia yeye ana maisha yake na kuwa hakuwahi kumhoji alipokwenda kwa Harmonize.



Filamu ya maisha halisia  ‘Behind The Gram’ inayomhusisha muigizaji Kajala Masanja na bintiye Paula Paul inaendelea kwenye Zamaradi TV.

Katika kipindi cha hivi punde, kutoka siku za nyuma, wawili hao walikabiliana kwa maneno baada ya Paula kumwalika aliyekuwa mpenzi wake wa wakati huo, Rayvanny kwenye kikao cha kambi ambacho kilikusudiwa kuwa cha familia tu.

Kajala alionekana akikimbia kwenye hema la Paula huku akiwa amefura kwa hasira kabla ya kumuuliza alikuwa na nani mle ndani.


"Paula, Paula. Hebu niambie nini kimefanyika? Nani huyo nimeona akitoka hapa sasa hivi? Niko serious. Nani amekuwa hapa," Kajala Masanja alisikika kujawa na ghadhabu alisikika akimuuliza binti yake Paula.

Katika majibu yake, mwanamitindo huyo mwenye umri wa miaka 20 kwa ujasiri alimwambia mama yake kwamba ni mwanamuziki Rayvanny ambaye alikuwa naye kwenye hema yake. 

Kajala aliyejawa na hasira alimkumbusha kuhusu mipango ya kikao hicho na kumuuliza kwa nini alichukua hatua ya kumwalika bosi huyo wa NLM.

"Dada (dadake aliyeandamana naye) tumekuja huku kufanya nini, na tulitakiwaa kuja wangapi labda, na kwa nini umlete Ray wakati unajua mimi nipo. Kwa hivyo hujali kunihusu," Kajala alimfokea bintiye.

Paula alimjibu mamake kwa kumkumbusha kuwa pia yeye ana maisha yake na kuwa hakuwahi kumhoji alipokwenda kwa Harmonize.

"Mimi nilikuacha ukaenda kwa Harmo, nikakaa mwenyewe. Na mimi niko na maisha yangu. Wewe ulijali," Paula alijibu.

Kajala alionekana kutopendezwa na majibu ya bintiye na alikuwa tayari kumpiga kabla ya dada yake aliyekuwa nao kuwazuia wasipigane. Aliwaambia hakuna haja ya kupigana na kumuomba Paula amheshimu mama yake.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad